Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba (P2)

Watu wengi hasa vijana watakuwa wanafahamu dawa ambazo hutumiwa sana kuzuia ujauzito pale ambapo wapenzi wamejamiiana ndani ya siku za hatari. Dawa hizi zipo za aina nyingi kama vile, P2, Morning After Pill na kadhali.

Endapo wawili hawa wanakuwa hawapo tayari kupata mtoto, na wanaona kwamba siku walizojamiiana zitapelekea mwanamke huyo kutunga mimba, basi anaweza kutumia p2 ambayo inaharibu mazingira au uwezekano wa mimba kutungwa.

Dawa hizi zinaweza kutumika ndani ya saa 72 tangu mwanamke alipojamiina, lakini ikumbukwe kuwa, kadiri unavyozitumia mapema, ndivyo uwezekano wake wa kuzuia mimba unavyozidi kuwa mkubwa.

Licha ya kuwa watu wengi hutumia dawa hizi, ni wachache sana huchukua muda na kutaka kujua madhara yatokanayo na dawa hizo. Kwa ufupi tutaangalia madhara yanayoweza kutokana na dawa hizo. Hii haina maana kwamba, ukiitumia, basi ni lazima madhara haya yote yatakayojadiliwa hapa yakutokee, bali yanaweza kutokea baadhi au yasitokee kabisa.

Dawa hizi husababisha madhara kwa baadhi ya watumiaji. Miongoni mwa madhara ya kawaida ambayo husababisha ni pamoja na kupata maumivu ya tumbo, kuvurugika kwa mfumo wa hedhi, kutapika.

Unapotumia dawa hizi, mfumo wa hedhi katika mwezi unaofuata, hedhi inaweza kuanza mapema zaidi au kwa kuchelewa na damu inayotoka inaweza kuwa nzito ama nyepesi kuliko ilivyo kawaida.

Madhara haya ni ya muda mfupi tu, yanapita. Unapotapika ndani ya saa 3 baada ya kumeza dawa hizi, unashauriwa kuonana na mtaalamu wa afya au umeze tena dawa hizo.

Madhara mengine yanayoweza kutokana na dawa hizi ni maumivu ya kichwa, kuumwa na nyonga, maumivu ya mgongo na misuli.

Unapotumia dawa hizi na kuhisi maumivu makali, unaweza kutumia dawa za kutuliza maumivu. Pia unaweza kula chakula au kitu kingine ili kupunguza maumivu ya tumbo.

Bado hakuna ushahidi wa kitaalamu kuwa matumizi ya dawa hizi yanaweza kusababisha madhara ya muda mrefu kwenye afya ya uzazi ya mtumiaji. Aidha, unashauriwa kutozitumia mara kwa mara.
Name

Afya Magazeti Makala Mapenzi Matukio Michezo News Siasa Udaku Urembo Wasanii
false
ltr
item
www.yanayojiri.com: Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba (P2)
Madhara ya kutumia dawa za kuzuia mimba (P2)
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSZoCYcv_CqsmVaZfRYLdE8dzGG-sbl4gy5LBKNaknfDPq-oz0z5tOZlTR4L9b9LzXJtvrq2XGkw21Bxay7MkBJxtL-FCgeUQ7ac23dnHW_oIlowM7VIDUodHklNnbqF3LPKptjNPvTX4/s640/file.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSZoCYcv_CqsmVaZfRYLdE8dzGG-sbl4gy5LBKNaknfDPq-oz0z5tOZlTR4L9b9LzXJtvrq2XGkw21Bxay7MkBJxtL-FCgeUQ7ac23dnHW_oIlowM7VIDUodHklNnbqF3LPKptjNPvTX4/s72-c/file.jpg
www.yanayojiri.com
http://nipasheapp.blogspot.com/2018/09/madhara-ya-kutumia-dawa-za-kuzuia-mimba.html
http://nipasheapp.blogspot.com/
http://nipasheapp.blogspot.com/
http://nipasheapp.blogspot.com/2018/09/madhara-ya-kutumia-dawa-za-kuzuia-mimba.html
true
3144336648072757917
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy
© Copyright www.yanayojiri.com | Designed By Me